Vurugu huko Roma baada ya Kura yenye Utata
Katika maandamano makali zaidi ya Roma tangu miaka ya 1970, waandamanaji 50,000 waliingia mitaani baada ya Waziri Mkuu wa Italia Silvio Berlusconi kunusurika chupuchupu hatua ya kumwondoa madarakani. Zaidi ya watu 100 walijeruhiwa.
Mapigano yalizuka kwa mara ya kwanza kati ya wanasiasa wasiokukubaliana katika jengo la Bunge, na mara tu matokeo ya kura yalipowekwa hadharani, waandamanaji walichoma moto magari, wakawashambulia maafisa wa polisi kwa baa za chuma, na kuharibu maduka ya eneo hilo. Kwingineko nchini, waandamanaji walivamia jengo la Soko la Hisa la Milan.
Bwana Berlusconi alishinda kwa kura tatu katika baraza la chini la Bunge, licha ya kupungua kwa umaarufu kutokana na pendekezo lake la kupunguzwa kwa bajeti, na madai ya ufisadi wa kisiasa, mashtaka ya kutokuwa na uwezo, na kashfa za ngono.
Waziri mkuu alisema Bunge lililo karibu halitasimamisha mipango ya chama chake kupunguza matumizi ya serikali.
"Tutasonga mbele kuhakikisha utulivu wa nchi," alisema (Financial Times).
Maandamano ya ziada, sawa na ghasia zinazoendelea nchini Ugiriki, Uingereza na Ufaransa, yanatarajiwa ikiwa hatua za kubana matumizi za Bwana Berlusconi zitatekelezwa.


